JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) ina jukumu la kukuza upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyohudumiwa vya kutosha na yasiyofikiwa kabisa na huduma za mawasiliano.

Katika kuhakikisha mikakati hii inafikiwa, TCRA inatekeleza mradi wa kugawa vifaa vya TEHAMA ambao unahakikisha jamii zisizofikiwa au zenye huduma duni za mawasiliano zinawezeshwa kupata vifaa na miundombinu.

Mradi wa vifaa vya TEHAMA unajumuisha utoaji wa vifaa hivyo kwa shule na uanzishaji wa vituo vya kutoa huduma za mawasiliano. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, mradi huu umehudumia jumla ya shule 34 na vituo vya kutoa huduma za mawasiliano 15 ambavyo vimeanzishwa hadi sasa. Shule au jamii zilizochaguliwa hupewa vifaa ambavyo ni pamoja na; 
i. Kompyuta 
ii. Printa na vichapishi 
iii. Utoaji wa intaneti (huduma za data)
Tangu kuanzishwa kwake, mradi huu umebadilisha jamii zilizohudumiwa kwa kuongeza idadi ya watu wanaotumia kompyuta, kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa njia za kidijiti, na kuongeza matumizi ya simu za mkononi. 

 

 

Je, una Maswali yoyote juu ya Sekta ya Mawasiliano?
Tuma Mrejesho na Malalamiko!

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imejidhatiti kutoa huduma bora kwa wateja na wadau wake wote.

Tuma Mrejesho na Malalamiko!