Mwanzo
Kuhusu
Huduma
Viunganishi
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

Programu ya Kusaidia Jamii

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, kama Taasisi huru ya Serikali, inaelewa na inaamini ya kwamba, kuwa na mafanikio kunakuja na jukumu la kurudisha kwa jamii kwa njiaya maana na endelevu.TCRA inaunga mkono juhudi na uwajibikaji katika kurudisha kwa kijamii kwasababu jambo hili linakusudia kuboresha maisha ya Watanzania,kupitia kupunguza umaskini na kukuza maendeleo ya uchumi kupitia matumizi ya TEHAMA. Mamlaka imechagua maeneo muhimu ambayo yatazingatiwa kwenye kutoa msaada. Maeneo haya ni anuwai ya kutosha kuhudumia mahitaji ya wanajamii ambayo yanaenda sambambana majukumuya Mamlaka ya MawasilianoTanzania.

Programu ya kusaidia jamii ya TCRA inazingatia maeneo mawili (2);
1.Maendeleo ya sekta ya Mawasiliano
2.Elimu

Maeneo haya pia yanaenda sambamba na Vipaumbele vya Maendeleo ya Kitaifa ya Tanzania. TCRA itahusika katika ushirikiano na washirika wa kuaminika wa ndani na wa kimataifa au mashirika ya kijamii ili kuongeza uwekezaji katika mipangoya maendeleo ya jamii inayozingatia kukuza TEHAMA.

TCRA imejikitakuhakikisha kuwa Uendelevu, Uwajibikaji na Uwazi unazingatiwa vizuri. Mamlaka itawasiliana na jamii na wadau ili kukuza sura chanya ya taasisina kuboresha sifaya Mamlaka kwa jamii.  

       

      

© 2023 TCRA, Haki zote zimehifadhiwa.