Mwanzo
Kuhusu
Huduma
Viunganishi
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAASISI YENYE VIWANGO VYA ISO 9001: 2015

Idara ya Huduma za Taasisi

  1. Kuanzisha na kuratibu utekelezaji wa Sera na Taratibu za Kifedha na rasilimali Watu;
  2. Kuanzisha Taratibu, Sheria, Miongozo, na Kanuni kwa ajili ya usimamizi mzuri na wenye ufanisi wa rasilimali watu na fedha kwenye Mamlaka;
  3. Kuanzisha Sera na Taratibu kwa ajili ya mifumo mizuri na yenye ufanisi ya Usimamizi;
  4. Kutoa ushauri wa kitaalamu na kiufundi kuhusiana na usimamizi wa kifedha kwenye Mamlaka;
  5. Kusimamia maandalizi na utekelezaji wa Mikakati ya Mamlaka na Mipango ya Utekelezaji ya Mwaka na Bajeti na kufanya mapitio ya katikati ya mwaka ya Mpango Mkakati na bajeti;
  6. Kufuatilia na kufanyia tathmini utekelezaji wa Mipango Mkakati ya Mwaka ya Mamlaka;
  7. Weka viwango, michakato na vigezo vya taratibu za utendaji kazi kwa ajili ya Usimamizi wa Rasilimali Watu kupitia uanzishaji wa kanuni za Mamlaka zinazohusu Wafanyakazi na Fedha, Mwongozo wa Uhasibu;
  8. Kuratibu shughuli za Ukaguzi wa Nje na ndani ya Mamlaka;
  9. Kutumika kama Katibu kwenye Kamati za Uteuzi, Nidhamu na Mapitio;
  10. Kusimamia maandalizi yote ya Ripoti za utendaji kazi za Mamlaka;
  11. Kuandaa Ripoti za Menejimenti katika maeneo ya Usimamizi wa Rasilimali watu na Fedha, Kutoa Huduma za Kiutawala na Utekelezaji wa jumla wa Mipango ya Mamlaka;
  12. Kuratibu maendeleo ya mipango na bajeti ya muda mrefu na mfupi ya Mamlaka na kusimamia utekelezaji wake;
  13. Kuratibu mara kwa mara tathmini ya Utendaji kazi ya Mwaka kulingana na maofisa waliomo kwenye Kurugenzi;
  14. Kusimamia Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji na Miradi ya Mamlaka;
  15. Kutoa huduma za ITU.
© 2023 TCRA, Haki zote zimehifadhiwa.