Idara ya Huduma za Taasisi
- Kuanzisha na kuratibu utekelezaji wa Sera na Taratibu za Kifedha na rasilimali Watu;
- Kuanzisha Taratibu, Sheria, Miongozo, na Kanuni kwa ajili ya usimamizi mzuri na wenye ufanisi wa rasilimali watu na fedha kwenye Mamlaka;
- Kuanzisha Sera na Taratibu kwa ajili ya mifumo mizuri na yenye ufanisi ya Usimamizi;
- Kutoa ushauri wa kitaalamu na kiufundi kuhusiana na usimamizi wa kifedha kwenye Mamlaka;
- Kusimamia maandalizi na utekelezaji wa Mikakati ya Mamlaka na Mipango ya Utekelezaji ya Mwaka na Bajeti na kufanya mapitio ya katikati ya mwaka ya Mpango Mkakati na bajeti;
- Kufuatilia na kufanyia tathmini utekelezaji wa Mipango Mkakati ya Mwaka ya Mamlaka;
- Weka viwango, michakato na vigezo vya taratibu za utendaji kazi kwa ajili ya Usimamizi wa Rasilimali Watu kupitia uanzishaji wa kanuni za Mamlaka zinazohusu Wafanyakazi na Fedha, Mwongozo wa Uhasibu;
- Kuratibu shughuli za Ukaguzi wa Nje na ndani ya Mamlaka;
- Kutumika kama Katibu kwenye Kamati za Uteuzi, Nidhamu na Mapitio;
- Kusimamia maandalizi yote ya Ripoti za utendaji kazi za Mamlaka;
- Kuandaa Ripoti za Menejimenti katika maeneo ya Usimamizi wa Rasilimali watu na Fedha, Kutoa Huduma za Kiutawala na Utekelezaji wa jumla wa Mipango ya Mamlaka;
- Kuratibu maendeleo ya mipango na bajeti ya muda mrefu na mfupi ya Mamlaka na kusimamia utekelezaji wake;
- Kuratibu mara kwa mara tathmini ya Utendaji kazi ya Mwaka kulingana na maofisa waliomo kwenye Kurugenzi;
- Kusimamia Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji na Miradi ya Mamlaka;
- Kutoa huduma za ITU.