Serikali imeweka Sheria na Kamati ya Maudhui yenye jukumu la kufuatilia maudhui ya Utangazaji yakiwemo maudhui ya wenye leseni za maudhui mtandaoni.
Kamati ya Maudhui hubainisha makosa katika maudhui ya utangazaji na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria. Pia, maudhui yenye sura ya jinai hufuatiliwa na kupepelezwa na Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Makosa ya Mtandao na kwa kutumia Sheria ya Makosa Mtandaoni. Jeshi la Polisi limekuwa likichukua hatua kwa watumiaji huduma za Mawasiliano wanaobainika kutumia isivyo huduma za Mawasiliano.
Taasisi ya Kuzuia na Kupambambana na Rushwa Tanzania-TAKUKURU ni taasisi ya serikali iliyopewa jukumu la kupambana na rushwa. Hivyo mwananchi anapaswa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa Taasisi husika ili kudhibiti vitendo vya rushwa.
TCRA tayari imeboresha na kuhuisha Kanuni za Utangazaji, ambapo gharama za leseni kadhaa zimefutwa na nyingine kupunguzwa. Masuala ya kodi zinazosimamiwa na Mamlaka nyingine za kikodi, hushughulikiwa na Mamlaka husika.



