- Unatoa njia muafaka na rahisi kwa Serikali na taasisi zake kuwasiliana na mwananchi kwa makusudi mbalimbali.
- Mfumo utarahisisha ufanyaji biashara ikiwa ni pamoja na za mtandao kwa wawekezaji wadogo hata wakubwa kwa vile biashara zitajulikana ziliko.
- Uandikishaji wa mali kama magari, biashara,wapiga kura utakuwa wa uhakika zaidi
- Njia rahisi ya kufanya utafiti kama sensa, sampuli za savei nk.
- Kuongeza utalii. Watapanga safari zao kuja nchini kwa ubora zaidi.
- Ufanisi katika shuguli za uokoaji majanga ya moto, magonjwa ya mlipuko, maafuriko na ajali.
- Itaongeza ubunifu kaatika matumizi ya intaneti na TEHAMA kwa ajili ya kutengeneza programu za kuongoza magari (GPS) na kusanifu ramani zinazotumika.
Mamlaka za Serikali za Mtaa ndizo zenye jukumu la kugawa na kusajili anwani wa wananchi wa eneo husika. Kwanza mtaa au barabara anayoishi mwananchi hutambuliwa na kuwekewa nguzo kuwa ina jina gani. Anwani ya makazi inagawiwa kwa mwananchi mwenye nyumba yake ambapo nyumba inapewa namba kutokana na barabara au mtaa ilipo. Aidha mlango wa mbele ya nyumba ndipo nambari ya nyumba itabandikwa upande wa kulia wa mlango ili ionekane.
Ndugu Lwitiko Ambele
4 Mtaa wa Mwakaleli
53122 Mwakibete
MBEYA
Postikodi pia hujulikana kama PIN Code nchini India,ZIP Code nchini Marekani, Postikodi nchini Canada na NPA katika nchi ya Uswizi inayoongea Kifaransa)
- Postikodi ni namba ya kiposta ambayo hutumika kutambulisha kwa usahihi eneo la utawala ambalo wananchi wanaishi.
- Postikodi ikitumika kwenye anwani humtambulisha mwananchi alipo kwa usahihi zaidi.
- Postikodi ni kitu chenye thamani katika nchi (rasilimali) na hutumika na wadau wengi kurahisisha shughuli za kibiashara.
Jukumu la kusajili namba za nyumba ni la Mamlaka za Serikali za Mitaa. Namba za nyumba zitawekwa kwa mfumo ufuatao:-
- Kuanzia mwanzo wa mtaa upande wa kushoto itaanza nambari 1 na kulia nambari 2;
- Kwenye mduara namba zitazunguka kuanzia kushoto kwenda kulia;
- Sehemu zisizopangwa namba zitafuata mitaa kwa tafisiri ya Tawala za Mikoa.
- Mfumo wa anwani kwa kutumia nambari za nyumba, jina la mtaa au barabara na postikodi. Kwa mfumo huu anwani inatolewa kwa kila mwananchi
- Mpango huu unahusu utambuzi na uwekaji wa majina ya mitaa, barabara na namba za nyumba.
- Lengo kuu: Kutoa anwani ya uhakika kwa kila kaya na sehemu za biashara au huduma nchini kote ili kumfikia mwenye anwani kwa uhakika zaidi.



