EMF "ElectroMagnetic Fields" ni dhana inayohusiana na sumaku-umeme. Vifaa vyote vya umeme au elektroniki vinazalisha sumaku-umeme. Vyanzo vya kawaida vya EMF ni pamoja na kompyuta, televisheni, ovena za maikrowevu, vifaa visivyotumia waya kama simu za mkononi na vifaa vya Wi-Fi, laini za umeme, mifumo ya waya katika majumba, paneli za umeme, transfoma, mota na aina zote za mifumo ya utangazaji, ikiwa ni pamoja na redio za AM na FM.
Pia, masafa na mifumo ya mwanga ya kawaida ni aina za EMF. Mbali na mwanga wa kawaida unaoonekana, aina nyingine za mwanga zisizoonekana kama vile mialekundu (infrared), na Urujuanimno (ultraviolet), eksrei na mionzi ya gamma ni aina za EMF.
Masafa ya redio, yanayofahamika pia kama “Radio Frequency – RF,” ni aina ya nishati ya sumaku-umeme inayozalishwa kwa kutumia Masafa ya juu kupitia vifaa vikubwa visivyohitaji muunganisho wa waya ili kuwezesha usafirishaji wa data.
Vyanzo vikuu vya RF ni pamoja na: miundombinu ya kurusha mawimbi ya masafa na televisheni, minara na antena za simu, simu zinazobebeka, simu za mkononi, mitandao ya kompyuta isiyo na waya (WLAN), na vifaa vya rada. Aidha, mifumo ya mawasiliano isiyo na waya inayotumika majumbani na kwenye majengo mbalimbali pia ni vyanzo vya RF.
RF EMF yaani "Radiofrequency Electromagnetic Fields" ni istilahi inayotumika kufafanua kiwango cha sumaku-umeme kinachojumuisha masafa kuanzia wigo wa kilohertz 100 (kHz) hadi Gigahertz 300 (GHz). RF EMF hutumika katika teknolojia mbalimbali, zaidi kwa madhumuni ya mawasiliano (kwa mfano simu za mkononi, vituo vya ubadilishanaji mawasiliano, Wi-Fi, 5G, redio, Luninga, vifaa vya usalama).
RF EMF pia hutumika katika tiba (kwa mfano mashine za uchunguzi wa afya za MRI), vifaa vya kupasha joto chakula (kwa mfano maikrowevu) na vifaa vya uhamishaji wa nishati bila waya (kwa mfano Qi).
Nchi mbalimbali huweka viwango vyao vya kitaifa vya mionzi (exposure) vinavyohusiana na sumaku-umeme.
Hata hivyo, sehemu kubwa ya viwango hivyo hutegemea miongozo iliyowekwa na Tume ya Kimataifa ya Ulinzi dhidi ya Mionzi isiyokuwa ya Ionizi (ICNIRP). Shirika hili lisilo la kiserikali, lenye uhusiano rasmi na Shirika la Afya Duniani (WHO), hufanya tathmini ya matokeo ya kisayansi kutoka nchi mbalimbali duniani. Kwa kuzingatia msingi wa mapitio ya kina ya maandiko ya utafiti, ICNIRP huandaa miongozo inayopendekeza viwango salama vya mionzi wa sumaku-umeme.
Miongozo hii hupitiwa mara kwa mara na kuboreshwa inapobidi.
Ndiyo. Kuna kiwango cha juu cha usalama kwa mionzi ya EMF kinachopendekezwa na Tume ya Kimataifa ya Ulinzi Dhidi ya Mionzi Isiyo ya Ionizi (ICNIRP).
ICNIRP hutumia kipimo cha usalama cha kuzidisha mara kumi (10) ili kupata kiwango cha juu cha mionzi kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye mazingira ya mionzi ya EMF na kuzidisha mara hamsini (50) kwa ajili ya kuweka kiwango kinachofaa kwa umma.
Ndiyo. Miongozo iliyotolewa na ICNIRP kuhusu viwango vya mionzi ya EMF imeandaliwa kwa kutumia uchambuzi makini wa utafiti wa kisayansi.
Lengo ni kuhakikisha ulinzi kwa watu wote, wakiwamo watoto na wanawake wajawazito, dhidi ya athari za kiafya zinazoweza kutokea kutokana na mionzi ya EMF. Kwa mujibu wa miongozo ya ICNIRP ya mwaka 2020, wanawake wajawazito wanaofanya kazi katika mazingira yanayohusisha Masafa ya RF wanashauriwa kuepuka kuwa kwenye mazingira yanayozidi kiwango cha mionzi kilichowekwa kwa ajili ya umma, ili kuhakikisha usalama wa ujauzito wao.
Si katika mazingira yote. Vipandikizi vya kielektroniki kwa kawaida huambatana na taarifa za kiusalama kuhusu hatari au uwezekano wa vifaa hivyo kuathiriwa na mwingiliano wa vifaa vya umeme na kielektroniki ikiwa ni pamoja na simu za mkononi na vifaa vinavyotumia masafa.
Vipo viwango maalumu vilivyowekwa kuhusu kinga dhidi ya mionzi ya masafa na mwingiliano wa masafa. Watu wenye vipandikizi vya kielektroniki wanapaswa kushauriana na wataalamu wao wa tiba kuhusu athari zinazoweza kusababishwa na mwingiliano wa masafa, hasa ikiwa wanapata wasiwasi kuhusu usalama wao. Miongozo ya ICNIRP kuhusu mionzi ya EMF haina kipengele kuhusu kinga dhidi ya mwingiliano wa vifaa vya kielektroniki.
Viwango mahsusi vya ufyonzwaji wa RF “Specific absorption rate (SAR)” ni kipimo cha kiwango cha nguvu ya RF ambayo hufyonzwa na tishu za mwili wa binadamu na hupimwa kwa kipimo cha wati kwa kilogramu(W/Kg). Upimaji huu hutumika kubaini ikiwa simu inakidhi viwango na au miongozo ya usalama.
Hili ni swali ambalo Shirika la Afya Duniani (WHO) wanalichukulia kwa uzito mkubwa. Ikizingatiwa idadi kubwa ya watu wanaotumia simu za mkononi, hata mabadiliko kidogo tu yenye kusababisha athari hasi kwa afya ya binadamu linaweza kuwa na athari kubwa kwa afya ya umma.
Ikizingatiwa kuwa mionzi ya masafa ya redio (RF) inayotolewa na simu za mkononi ni zaidi ya mara elfu moja (x1000) kuzidi ile inayotokana na minara ya mawasiliano na kwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa athari kubwa zaidi kutokana na matumizi ya vifaa hivi vya mkononi, tafiti zimekuwa zikifanyika kwa umakini mkubwa kuchunguza madhara yanayoweza kutokea. Utafiti huu umelenga maeneo yafuatayo:
- Uwezekano wa kusababisha saratani
- Athari nyinginezo za kiafya
- Mwingiliano wa sumaku-umeme
- Ajali za barabarani zinazohusiana na matumizi ya simu za mkononi.
Saratani
Utafiti wa kiepidemiolojia unachunguza uhusiano kati ya mionzi ya RF itokanayo na simu za mkononi na hatari ya kupata aina fulani za saratani ya kichwa, kama vile glioma na neuroma. Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Saratani (IARC) limeainisha masafa haya ya mionzi kama yenye uwezekano wa kusababisha saratani kwa binadamu, na kuyaweka katika Kundi 2B. Ingawa tafiti zilizopo hadi sasa hazionyeshi ushahidi thabiti kwamba mionzi ya RF kutoka kwa minara ya mawasiliano inaongeza hatari ya saratani au magonjwa mengine.
Athari Nyingine za Kiafya Zinazohusiana na Matumizi ya Simu za Mkononi
Watafiti wamebaini athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya simu za mkononi, ikiwa ni pamoja na mabadiliko katika shughuli za ubongo, athari kwenye stimuli za mrejesho na mifumo ya usingizi. Ingawa athari hizi zinaonekana kuwa ndogo na hazijaonyesha madhara makubwa ya kiafya, utafiti zaidi unahitajika ili kuthibitisha matokeo haya.
Muingiliano wa Umeme Sumaku
Muingiliano wa Umeme sumaku kati ya simu za mkononi na vifaa vya matibabu kama vile vifaa vya kuweka mapigo ya moyo (pacemakers), vichochezi vya moyo vinavyopandikizwa na baadhi ya visaidizi vya kusikia unaweza kuwa na athari katika utendaji kazi wa vifaa hivyo. Simu za mkononi zinapowekwa karibu mno na vifaa hivi, zinaweza kutoa mawimbi ya umeme sumaku ambayo yanasumbua mawimbi ya kawaida yanayotumika na vifaa hivi vya matibabu. Athari hizi zinaweza kupunguzwa kwa kutumia teknolojia mpya zaidi kama vile simu za 3G au zaidi, ambazo zimeundwa kutoa mawimbi yenye nguvu ndogo zaidi ya kuingiliana na vifaa vya matibabu. Kadhalika, kuna muingiliano unaoweza kutokea kati ya masafa ya simu za mkononi na mawasiliano ya kielektroniki ya ndege, jambo ambalo limepelekea baadhi ya nchi kuweka sheria na kanuni zinazodhibiti matumizi ya simu za mkononi ndani ya ndege. Hata hivyo, kuna ndege zingine ambazo zinatumia mifumo maalumu inayoweza kudhibiti athari hizi, hivyo kuruhusu matumizi ya simu za mkononi wakati wa safari bila kuathiri mifumo ya ndege.
Ajali za Barabarani
Utafiti unaonyesha kuwa matumizi ya simu za mkononi wakati wa kuendesha chombo cha moto, iwe kwa kushikilia au kwa kutumia vifaa vya kuwasiliana bila kushikilia, husababisha ongezeko la ajali za barabarani mara tatu hadi nne zaidi ya kawaida. Ajali hizi husababishwa na ghasia zinazotokana na matumizi ya simu.
Hitimisho
Ingawa bado haijathibitishwa kama matumizi ya simu za mkononi yanaongeza hatari ya uvimbe kwenye ubongo, ongezeko la matumizi ya simu hizi na upungufu wa data za kisayansi kuhusiana na matumizi ya vifaa hivi vya mawasiliano kwa zaidi ya miaka 15 yanasisitiza umuhimu wa utafiti zaidi. Hii ni muhimu hasa kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya simu za mkononi miongoni mwa vijana wadogo ambao wanaweza kuwa wazi kuguswa na athari za mionzi ya ‘RF’ kwa muda mrefu zaidi, hivyo kuongeza hatari ya athari hasi. Shirika la Afya Duniani (WHO) linapendekeza utafiti zaidi kufanyika juu ya athari za kiafya za mionzi ya ‘RF’, hasa kwa kundi hili la watumiaji na kwa sasa linaendelea kuchambua athari hizi kwa vipimo vinavyostahili kuzingatiwa.
5G, au kizazi cha tano, ni teknolojia ya hivi karibuni ya simu za mkononi isiyotumia waya, ambayo ilianza kutumiwa kwa wingi mnamo mwaka 2019. Inatarajiwa kwamba 5G itaongeza utendaji kazi na aina mbalimbali za matumizi mapya ya teknolojia za kidijiti, ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za afya kwa masafa ‘telemedicine’, ufuatiliaji wa afya wa kina, upasuaji wa masafa.
5G inaleta mapinduzi katika viwango vya mawasiliano ya simu za mkononi kwa kuleta utendaji ulioboreshwa kwa kiasi kikubwa. Teknolojia hii inapanua matumizi ya masafa ya mawimbi ya redio kutoka takriban 3.5 GHz hadi masafa ya juu ya makumi ya GHz. Masafa haya ya juu ambayo ni mapya katika mitandao ya simu za mkononi, tayari yanatumika katika matumizi mengine kama vile muunganisho wa vifaa vinavyounganisha nukta moja na nyingine na skana za ukaguzi. Katika masafa haya ya juu, mitandao ya 5G inahitaji minara zaidi na vifaa vingi vilivyounganishwa ili kuhakikisha ufanisi na kasi. Zaidi ya hayo, 5G inatumia teknolojia ya antenna za beam-forming, ambazo zinaweza kuelekeza mawimbi ya masafa moja kwa moja kwenye kifaa kinachotumia mtandao, tofauti na antena za minara zinazotumika katika mitandao ya zamani kama 3G na 2G ambazo zinasambaza masafa kwa upana zaidi. Hii inaruhusu matumizi bora ya masafa na kuongeza kasi na ufanisi wa mawasiliano.
Viwango vya Mionzi
Kwa sasa, mionzi inayotolewa na miundombinu ya 5G kwenye masafa ya 3.5 GHz inalingana na ile inayotokana na minara ya simu za teknolojia za zamani, kama vile 2G, 3G na 4G. Kutokana na matumizi ya masafa mapana zaidi na antena za 5G, kiwango cha mionzi kinaweza kubadilika kulingana na eneo la watumiaji na jinsi wanavyotumia teknolojia hiyo. Ikizingatiwa kwamba teknolojia ya 5G bado iko katika hatua za awali za usambazaji, athari za mabadiliko yoyote yanaweza kutokea kutokana kuwa kwenye wigo wa Masafa ya Redio yanaendelea kuchunguzwa.
Mpaka sasa, utafiti uliofanyika umeonesha kwamba hakuna madhara ya moja kwa moja ya kiafya yanayohusishwa na mionzi ya vifaa visivyotumia waya. Matokeo ya tafiti hizo kuhusu athari za kiafya yanatokana na uchunguzi uliolenga masafa maalumu pekee. Hata hivyo, tafiti chache tu zimefanywa kuhusu athari za kiafya za masafa yanayotumika katika teknolojia ya 5G. (Ikumbukwe: muktadha huu unahusisha masafa maalumu pekee).
Kuongezeka kwa joto katika tishu za mwili wa binadamu ni athari ya moja kwa moja inayotambuliwa kutokea kutokana na mwingiliano kati ya mawimbi ya masafa na mwili wa binadamu. Viwango vya mionzi kutokana na teknolojia zilizopo sasa hivi husababisha ongezeko dogo tu la joto mwilini. Kadri masafa yanavyoongezeka, kuna upenyo mdogo zaidi ndani ya tishu za mwili na ufyonzwaji wa nishati unazidi kuhusika zaidi na uso wa mwili (ngozi na macho). Izingatiwe kwamba viwango vya mionzi wa jumla vinabaki chini ya miongozo ya kimataifa; zingatia kwamba hakuna madhara yoyote kwa afya ya umma yanayotarajiwa.
Mashirika mawili ya kimataifa yamechukua jukumu la kuandaa miongozo inayohusiana na mionzi ya sumaku-umeme. Kwa sasa, nchi nyingi zinazingatia miongozo ifuatayo:
- Tume ya Kimataifa ya Ulinzi dhidi ya Mionzi isiyo ya Ki-ionizi (ICNIRP), na
- Taasisi ya Wahandisi wa Umeme na Elektroniki (IEEE), ambayo hutoa miongozo kupitia Kamati yake ya Kimataifa ya Usalama wa Sumaku-umeme.
Miongozo hii imeundwa ili kuhudumia teknolojia mbalimbali na sio teknolojia maalum pekee; inashughulikia masafa yote ya mawasiliano, hadi GHz 300. Hii ni pamoja na masafa yanayotumika katika teknolojia za 5G.
WHO lilianzisha Mradi wa Kimataifa wa Sumaku-umeme (EMF) mnamo mwaka 1996. Mradi huo unachunguza athari za kiafya za mionzi
ya umeme na sumaku katika masafa ya 0-300 GHz na hutoa ushauri kwa mamlaka za kitaifa kuhusu athari za mionzi ya EMF.
Ndiyo, simu za mkononi hutoa mionzi kwa kiasi kidogo chenye vinasaba vya masafa yanayowezesha mawasiliano.
Simu za mkononi hutumia transmita za nguvu ndogo sana ambazo hutoa nishati chini ya watts 2 kwa kiwango cha juu. Simu za mkononi zimebuniwa kwa namna ambayo zinaweza kufanya kazi kwa ubora huku zikitumia nishati ya kiwango cha chini kabisa. Uwezo huu hujulikana kama ‘udhibiti wa matumizi ya nishati unaoendana na hali’.



