Tovuti ya TZ-CERT, ambayo ni https://www.tzcert.go.tz/ inatoa taarifa kwa watumiaji wote na wasimamizi wa mifumo kuhusu tahadhari za usalama, ushauri, matangazo, miongozo na namna bora ya kushughulikia matatizo ya usalama.
Unaweza kupata kwa wakati taarifa za hivi karibuni kuhusu usalama kwa kujisajili ili kupata nakala ya jarida la TZ-CERT linalopatikana mtandaoni kupitia: https://www.tzcert.go.tz/subscribe-to-our-newsletter/.
Wakati wa kutoa taarifa ya tukio, ni muhimmu sana kutoa taarifa zilizo kamilika na kwa kina. Zinaweza kuwa na mambo yaliyoorodheshwa hapa chini au zaidi
- Jina la anayetoa taarifa na namna atakavyopatikana (mfano namba ya simu, anwani ya baruapepe).
- Namba inayoonyesha aina ya kifaa, namba ya kifaa, jina la anayehudumia tovuti ambao kifaa kimeunganishwa, anwani ya intaneti kama inaweza kufikiwa na watu wengi) na mahali ilipo.
- Tarehe na muda wa tukio.
- Maelezo ya kina kuhusu jambo lililotokea, ikiwa ni pamoja na namna kompyuta husika ilivyoshghulikiwa baada ya kugunguliwa tukio la kuwepo kirusi. Maelezo haya yawe kamili, yakiwa na nukuu ya maneno halisi yaliyoonyeshwa kwenye ujumbe wa tahadhari uliojitokeza kutoka kwenye programu ndogo ya malware au antivirus.
Taarifa ya tukio inaweza kutolewa kwa njia hizi:
- Kujaza kikamilifu na kuwasilisha fomu inayopatikana mtandaoni kwenye tovuti ya TZ-CERT Website ambayo ni:
- Kutuma barua pepe kwenda:
PGP Key id: EED630F6
PGP Fingerprint: 0A1C CF48 D623 9BE7 676B 4C03 EF91 6FCA EED6 30F6
Tukio la kimtandao ni kitu kimoja au mfululizo wa vitu visivyotakiwa na visivyotarajiwa ambavyo vina uwezekano mkubwa wa kuathiri shughuli na utendaji au kutiia usalama wa taarifa, ambapo “Usalama wa Taarifa” ni kuhifadhi Usiri, Uimara na Upatikanaji wa Taarifa.
TZ-CERT inatoa huduma zilizoorodheshwa hapa chini bila malipo yoyote kwa wadau wake na umma kwa ujumla:
- Kutoa tahadhari, Onyo na Matangazo
- Kuchukua hatua dhidi ya matukio
- Kutoa elimu kuhusu uelewa wa masuala ya usalama mtandaoni
- Kutathmini udhaifu wa mifumo na kufanya majaribio ya kuingilia mifumo
- Kuchambua Ushahidi wa kidijitali kuhusu mifumo
TZ-CERT kifupisho cha kiingereza cha Kitengo cha Dharura cha Kitaifa cha Kushughulikia Masuala ya Usalama wa Mitandao. Ni timu ya kitaifa yenye majukumu ya kuratibu matukio ya usalama katika mitandao kwenye ngazi ya taifa na kushirikliana na vyombo vingine vya kikanda na kimataifa vinavyojihusisha na kusimamia matukio ya usalama mitandaoni.



